Cristiano Ronaldo amewataka waamuzi duniani kote kuhakikisha wanawaweka wachezaji walinzi mbali na mpira wa adhabu ya moja kwa moja (free-kicks).
Nyota huyo wa Ureno na Real Madrid ni mmoja wa wapigaji wazuri wa pigo la aina hiyo duniani ambaye ametaka kufanyike mabadiliko ya sheria ambayo anadhani hiyo itamfanya aweze kuuzamisha mpira wavuni kupitia eneo la kona ya juu ya goli.
'Sheria ambayo itakuwa nzuri endapo itatumika popote ni kuwa wakati unapiga 'free-kick', mwamuzi aweke alama ya uzio kuhakikisha kuwa walizni wanakuwa mbali ' Amesema Ronaldo alipoulizwa katika mkutano wake na Dubai
International Sports .


Pichani juu mshambuliaji wa Real Madrid na Ureno akijiweka tayari kupiga 'free-kick' na anaamini kuwa badiliko sheria hiyo itamuwezesha kufunga magoli zaidi kwa klabu na timu yake ya taifa.

Tunzo: Ronaldo alikabidhiwa tunzo ya 'Global Soccer' katika mkutano wake mjini Dubai
NINI KINGINE WANGEPENDELEA KIBADILISHWE.
PEP GUARDIOLA, BAYERN MUNICH MANAGER
Kama kocha ningependelea kufanya mabadiliko mengi zaidi ya wachezaji, hii ingeniruhusu mimi kama meneja kuiongoza timun kwa uzuri zaidi. Itakuwa vizuri kuwa na wachezaji wengi katika benchi kwa kweliIt. Kila mmoja angenufaika na hii kwasababu wachezaji wangekuwa wanachoka kidogo pia.
FABIO CAPELLO, RUSSIA MANAGER
Tungekuwa na muda kuongea na wachezaji kila baada ya muda fulani 'timeout'. Ukiwa katika benchi huwezi kuongea kubabilisha mbinu, huwezi kutuma ujumbe. Nchini Russia, endapo mchezaji anaanguka tunakuwa na dakika moja ya kusimamisha mchezo kuwapa wachezaji nafasi ya kupumua.Linazungumzika hili.
ANTONIO CONTE, JUVENTUS MANAGER
Fabio ameiba wazo langu. 'timeout' lingekuwa ni wazo zuri sana kwasababu ukiwa katika benchi huwezi kuwasiliana na wachezaji. Endapo utagundua makosa, dakika mbili za kupumzika kwa kutoa maelekezo zingefaa sana.
Kama kocha ningependelea kufanya mabadiliko mengi zaidi ya wachezaji, hii ingeniruhusu mimi kama meneja kuiongoza timun kwa uzuri zaidi. Itakuwa vizuri kuwa na wachezaji wengi katika benchi kwa kweliIt. Kila mmoja angenufaika na hii kwasababu wachezaji wangekuwa wanachoka kidogo pia.
FABIO CAPELLO, RUSSIA MANAGER
Tungekuwa na muda kuongea na wachezaji kila baada ya muda fulani 'timeout'. Ukiwa katika benchi huwezi kuongea kubabilisha mbinu, huwezi kutuma ujumbe. Nchini Russia, endapo mchezaji anaanguka tunakuwa na dakika moja ya kusimamisha mchezo kuwapa wachezaji nafasi ya kupumua.Linazungumzika hili.
ANTONIO CONTE, JUVENTUS MANAGER
Fabio ameiba wazo langu. 'timeout' lingekuwa ni wazo zuri sana kwasababu ukiwa katika benchi huwezi kuwasiliana na wachezaji. Endapo utagundua makosa, dakika mbili za kupumzika kwa kutoa maelekezo zingefaa sana.
Ronaldo, mwenye magoli 40 katika jumla ya michezo 32 kwa klabu yake na timu ya taifa msimu huu alikuwa akiulizwa maswali na mwamuzi mstaafu na mkongwe Pierluigi Collina.
Pia alizwadiwa tunzo ya 'Global Soccer
Award ' ya mwaka 2013 katika mkutano huo 'conference'.
Bahati nzuri katika maoni ya Ronaldo ni kwamba shirikisho la soka dunia FIFA hivi karibuni lilithibitisha kuwa waamuzi watakuwa wakipewa 'spray maalumu' katika kombe la dunia na hiyo bila shaka litakuwa ni jibu la maoni yake.
Wachezaji kadhaa na mameneja walikuwepo katika Conference hiyo iliyofanyika Dubai, akiwemo bosi ya Bayern Munich Pep Guardiola, meneja wa Juventus
Antonio Conte na yule wa and Russia Fabio Capello.

Magic marker: FIFA imeamua kuanza kutumia 'biodegradable spray' katika kombe la dunia ilifanyiwa majaribio katika kombe la dunia la vilabu nchini Morocco

Wanakuna vichwa: meneja wa Juventus Antonio Conte
(kushoto), Meneja wa Russia Fabio Capello (katikati) na bosi wa Bayern Pep
Guardiola wote walikuwa na maoni yao katika 'conference' hiyo

Waalikwa: Mlinzi wa zamani wa Real Madrid na Blackburn Rovers Michel Salgado alikuwepo ndani ya conference

No comments:
Post a Comment