KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, December 31, 2013

Yanga yajitoa kombe la mapinduzi Ashant United kuchukua nafasi yake


Taarifa zinaeleza kuwa huenda Ashant United ikaelekea visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya kombe la mapinduzi baada ya kuthibitika kuwa mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga imejitoa kushiriki michuano hiyo. Taarifa za awali zinaeleza kuwa Yanga imeshindwa kuafikiana na waandaaji wa michuano hiyo kutokana na kile kilichoelezwa kuwa waandaaji wameshindwa kuwatumia barua rasmi ya ushiriki wao pamoja na maelezo ya kutosha juu ya malazi na makazi wakati wote wa mashindano.
Taarifa za hivi karibu zinaeleza kuwa kamati ya maandalizi inafanya mawasiliano na klabu ya Ashanti United ya Ilala jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuziba nafasi ya Yanga wakati huu ambapo michuano hiyo imepangwa kuanza kutimu vumbi hapo kesho.
Yanga ilikuwa imepangwa katika kundi C pamoja na Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Azam FC pamoja na makamu bingwa Tusker ya Kenya na Unguja Combine.
 Kwa mujibu wa ratiba ya michuano hiyo, pazia la michuano hiyo litafunguliwa kwa mechi mbili za kundi B katika uwanja wa Amaan, ambapo wakati wa saa 10:00 jioni ni mabaharia wa KMKM dhidi ya Kampala City Council (KCC) ya Uganda . Aidha saa 2:00 usiku, wekundu wa Msimbazi Simba SC, watakuwa kibaruani dhidi ya AFC Leopards. Januari 2, 2014, kutakuwa na mechi nne, katika kila uwanja, kati ya Amaan Unguja na  Gombani Pemba, kutakuwa na michezo miwili. Zile za Amaan, ni kati ya Azam FC na Unguja Combine (saa 10:00 jioni) na Yanga( Ashanti) dhidi ya Tusker itakayorindima kuanzia saa 2:00 usiku, na huko Gombani shughuli itakuwa kati ya URA na Chuoni (kundi C) watakaovaana saa 8:00 mchana, huku Mbeya City ikitoana jasho na Pemba Combine, saa 10:00 jioni katika mchezo wa kundi A. Fainali ya ngarambe hizo itapigwa uwanja Amaan Januari 12 wakati wa saa 2:00 usiku, ambayo ndiyo kilele cha maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment