KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, January 21, 2014

League Cup: United wanasema watatoa zawadi kwa mashabiki wao hiyo kesho

Kombe la League Cup limeibuka kama nafasi ya mwisho ya mabingwa wa ligi ya Premier ya Uingereza, Manchester United, kuokoa msimu ambao unazidi kukumbwa na huzuni kila kuchao.

Huku uteteaji wa taji lao la ligi kuu ukisambaratika baada ya kuchakazwa 3-1 ugenini na Chelsea Jumapili na kuwaacha alama 14 nyuma ya viongozi, magwiji hao pia waling'olewa kutoka kombe la FA kwa kuabishwa 2-1 na Swansea. 

Ingawa michuano ya kombe la League Cup lilipuuziwa mara kwa mara na mtangulizi wa meneja, David Moyes, Sir Alex Ferguson, meneja huyo wa sasa hana budi kutumia viungo wake mahiri watakapo waalika Sunderland Old Trafford Jumatano.

United wana kibarua cha kupindua matokeo ya kichapo cha mabao 2-1 katika awamu ya kwanza ya nusu-fainali yao uwanja wa Stadium of Light.

“Tutafanya lolote ili kufuzu ili kuwapa mashabiki jambo la kusherehekea. Kumetokea masaibu mengi na ninafahamu hayo kikamilifu,” Moyes aliambia runinga ya klabu hicho, MUTV.

Meneja huyo ambaye amejiweka katika shinikizo baada ya kudorora kimatokeo katika kampeni hii ameshuhudia timu hiyo ikipoteza mechi nne kati ya tano tangu Januari 7.

Kiungo wake, Michael Carrick, amesema United hawana lingine ila kutafuta suluhu ya dharura kurejelea ushindi.

“Tuna hamu ya kurejea tena haraka iwezekanyavyo. Jumatano tuna kibarua kikubwa kwani ni nafasi ya kufuzu fainali ya michuano na hatupuuzii. Tutajiinua kutoka kupoteza katika mchezo dhidi ya Chelsea na tuko tayari kupambana Jumatano,” Carrick alisema. 

No comments:

Post a Comment