Young Africans kesho jumatatu saa 8 mchana kwa saa za nchini Uturuki
sawa na saa 9 kamili kwa saa za Afrika Mashariki itashuka dimbani
kucheza mchezo wake wa mwisho wa kirafiki dhidi ya timu ya Simurq PIK
inayoshiriki Ligi Kuu nchini Azerbajain katika viwanja vya Side
Manavgat.
Kocha mkuu wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Plyum amesema
watautumia mchezo huo kama sehemu ya mwisho ya maandalizi ya kujianda na
Ligi Kuu ambayo inatarajiwa kuanza mwishoni mwa wiki ijayo ambapo
watoto wa jangwani watafugua dimba dhidi ya Ashanti United uwanja wa
Taifa.
Mchezo wa kesho utakua mgumu pia, kwani timu ya Simurq PIK
ina wachezaji wazuri ambao wanatoka sehemu mbali mbali dunianina ipo
katika nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu nchini kwao, hivyo
nadhani kitakua kipimo kizuri cha mwisho kabla ya kurejea nchini
Tanzania
Akiongelea kikosi chake mara baada ya mazoezi ya asubuhi,
Hans amesema anashukuru mungu maendeleo ya timu ni mazuri, mabadiliko
yapo na wachezaji wanaonekana kumuelewa hivyo anaamini kadri siku
zinavyokwenda timu itakua katika kiwango kizuri zaidi.
"Nimeshashuhudia
michezo miwili mmoja tukishinda 2-0 dhidi ya timu ya Altay SK Lidi
Daraja la pili Uturuki na jana tukitoka sare ya 0-0 dhidi ya timu ya KS
Flumartari ya Ligi Kuu Albania, kwa kweli nawapongeza vijana wanaonyesha
kweli wanajua wajibu wao na kucheza kwa kufuata maelekezo ya walimu"
alisema Hans.
Aidha Hans amesema ni jambo njema timu imecheza
jumla ya michezo mitatu, ikishinda miwili na kutoka sare mchezo mmoja,
huku ikifunga mabao 5 na kutokuruhusu nyavu zake kutikisika hii yote
inayonyesha timu imeiva tayari kwa mashindano yanayotukabili.
Mpaka
sasa hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja kufuatia kiungo Hassan Dilunga
kupona malaria na kuungana na wenzake katika mazoezi.
No comments:
Post a Comment