KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 20, 2014

LIGI DARAJA LA KWANZA NETBALL: TIMU YA JKT MBWENI YATAWAZWA KUWA MABINGWA 2014/15

JKT Mbweni wametawazwa kuwa mabingwa wa michuano ya ligi daraja la kwanza 2014/2015 kufuatia ushindi wa magoli 32-23 dhidi ya timu ya Uhamiaji katika mchezo wa fainali uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma. Mbali na kikombe cha Ubingwa pia washindi wapya JKT Mbweni wamezadiwa shilingi laki nne kutoka kwa wadhamini kampuni ya vinywaji baridi ya Pepsi ambao pia walitoa fulana kwa washindi wa kwanza mpaka watatu. Anna Kibira mwenyekiti wa chama cha mchezo wa netball nchini Tanzania CHANETA amesema mashindano yalikuwa mazuri na kusisimua, ambapo amevishukurua vilabu vyote ambavyo vimeshiriki mashindano hayo ambao wamepokea vyeti vya ushiriki wao.

No comments:

Post a Comment