KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, December 2, 2013

Tuzo ya bbc nani bora Afrika: Aubameyang,Victor Moses, John Obi Mikel, Jonathan Pitroipa na Yaya Touré baadaye kidogo.

Mshindi wa tuzo ya BBC ya mwanasoka bora wa Afrika mwaka 2013, anatarajiwa kutangazwa Jumatatu, Desemba 2, 2013.
Mshindi huyo atatangazwa kwa wakati mmoja katika redio na televisheni ya BBC, Focus on Africa, saa mbili na dakika 35 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Idhaa ya Dunia ya BBC ilitangaza orodha ya wachezaji kutoka Afrika watakaowania tuzo ya BBC ya mwanasoka bora wa mwaka 2013 ijulikanayo kama "BBC African Footballer of the Year award".
Wachezaji waliotajwa na wataalam wa masuala ya soka kuwania tuzo hiyo ni:
1.Pierre-Emerick Aubameyang - mchezaji wa timu ya taifa ya Gabon na Borussia Dortmund ya Ujerumani.
2.Victor Moses - wa timu ya taifa ya Nigeria na Liverpool ya England akiwa katika mkopo kutoka timu ya Chelsea pia ya England.
3.John Obi Mikel - mchezaji wa timu ya taifa ya Nigeria na klabu ya Chelsea ya England.
4.Jonathan Pitroipa -mchezaji wa Burkina Faso na Rennes ya Ufaransa.
5.Yaya Touré - mchezaji wa timu ya taifa ya Ivory Coast na pia timu ya Manchester Cityya England.
Kazi ya kuwapigia kura wachezaji hao ilianza tarehe 11 Novemba 2013 saa nane na dakika arobaini na tano kwa saa za Afrika Mashariki, wakitangazwa katika kipindi cha asubuhi cha BBV cha Newsday.

No comments:

Post a Comment