KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 8, 2012

Keita aondoka Barcelona baada ya mataji 14 katika kipindi cha miaka minne.


Kiungo wa kimataifa wa Mali Seydou Keita ameondoka Barcelona baada ya kuwepo katika klabu hiyo katika kipindi cha mafanikio cha mataji lukuki ndani ya kipindi cha miaka minne ya utumishi wake ndani ya klabu hiyo.
Barcelona imetoa taarifa inayosomeka
"Seydou Keita ametangaza usiku huu hataendelea na klabu hii msimu ujao,".
"Barcelona inamshukuru Seydou Keita kwa mchango wake kwa miaka michache na inamtakia kila la kheri zaidi katika soka lake kama professional na mafanikio binafsi siku za baadaye."
Keita ambaye amefanikiwa kutwaa mataji 14 akiwa na Barca anahusishwa na kutaka kuelekea Uchina katika klabu ya Dalian Aerbin.

  REKODI YA KEITA YA MATAJI BARCA

    3 x Spanish league (2009, 2010, 2011)
    2 x Uefa Champions League (2009, 2011)
    2 x Copa del Rey title (2009, 2012)
    2 x Fifa Club World Cup (2009, 2011)
    2 x Uefa Super Cup (2009, 2011)
    3 x Spanish Super Cup (2009, 2010, 2011)
Safari ya wanasoka waafrika kuelekea Uchina imekuwa ikivuta nyota wengi ambapo sasa tayari Didier Drogba, Frederic Kanoute na Yakubu Aiyegbeni wote wamejiunga vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Uchina maarufu kama Chinese Super League.
Keita mwenye umri wa miaka 32 alijiunga Barcelona akitokea Sevilla mwaka 2008 na alikuwa ni mchezaji wa kwanza kusainishwa na aliyekuwa kocha wakati huo baada ya kujiunga na Barca Pep Guardiola.

 Taarifa toka Hispania zinasema Keita amekatisha mkataba wake ambao ulikuwa umalizike 2014 na ambao ungemruhusu kuondoka kama mchezaji huru.
Huko nyuma Keita kavitumikia vilabu kama Marseille, Lorient na Lens vyote vya nchini Ufaransa kabla yan kujiunga na Seville kwa msimu mmoja.

No comments:

Post a Comment