KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, November 26, 2012

CECAFA CHALENJI CUP: Rwanda 2-0 Malawi Zanzibar 0-0 Eritrea


Mabao mawili yaliyofungwa katika kila kipindi yametosha kuwapa ushindi wa mabao 2-0 timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’ dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi “The Flames” na hivyo kuanza vema kampeni ya kuwania taji la michuano ya ‘Cecafa Tusker Chalenji Cup 2012’mchezo wa kundi C uliopigwa katika dimba la Namboole.

Rwanda ilianza kulisakama lango la Malawi tangu mapema kunako dakika ya 8 kupitia kwa Jimmy Mbagara lakini hata alikuwa tayari mwamuzi wa pembeni alikuwa ashiria kuwa mfungaji alikuwa ameotea.

Jean Baptiste Muginereza hata aliamsha shamrashamra kwa mashabiki wa Amavubi kunako dakika ya 38 baada ya kunasa mpira wa krosi wa mlinzi wa Mwemere Ngiritushi.

Kabla ya goli hilo washambuliaji wa Malawi Joseph Kamwendo, Chimango Kayira na Green Harawa walikuwa wakishambulia ngome ya Rwanda lakini mlinda mlango wa Amavubi  Jean Claude Ndoli alikuwa alikuwa akifanya kazi ya ziada kuokoa michomo yao.

Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika huku mwamuzi Ali Kalyango alipopuliza filimbi ya kuashiria kuwa ni mapumziko Rwanda walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0.

Baada ya mapumziko, Malawi walirejea kwa ari kwa kusukumu mashambulizi katika ngome ya Rwanda huku wakipata kona tano ndani ya dakika chache za kipindi hicho cha pili.

Dakika ya 78 kiungo ‘skipper’  Haruna Niyonzimana aliandika bao la pili kwa mabingwa hao wa mwaka 1999 baada ya kazi nzuri ya kuwazunguka mabeki wa Malawi kabla ya kuachia shuti kali lilikwenda moja kwa moja upande wa kulia wa mlinda mlango wa Malawi.

Ushindi huo umewapa uongozi wa kundi C wakiwa na alama 3 na magoli mawili na Malawi wakiwa mkiani.
Katika mchezo wa mapema Eritrea na Zanzibar zilikwenda sare ya bila kufungana

No comments:

Post a Comment