KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, November 5, 2012

KIMATAIFA: FERGUSON ANASEMA IKITOKEA PENATI NYINGINE NITAPIGA MWENYEWE NA MANCINI AKATA TAMAA YA KUSONGA MBELE LIGI YA MABINGWA.



 Meneja wa mashetani wekundu Manchester United Sir Alex Ferguson ametoa kali ya mwaka baada ya kusema kuwa itakapo tokea timu yake kuzawadiwa penati basi atakwenda kupiga yeye mwenyewe hii ni baada ya mshambuliaji wake Wayne Rooney kukosa penati katika mchezo ambapo United iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Arsenal jumamosi.

Mabao ya Robin van Persie na Patrice Evra yalitosha kuwafanya mashetani wekundu kuzoa alama zote tatu muhimu katika mchezo huo na kujikita katika kilele cha msimamo wa ligi kuu ya England ‘Premier League’ kwa mara ya kwanza msimu huu.

Hata hivyo ushindi wa mabao hayo 2-1 ungekuwa mkubwa zaidi andapo Rooney angefanikiwa kufunga penati yake ambayo ilitoka nje penati ambayo ilitokana na Santi Cazorla kuunawa mpira katika eneo la hatari.

Rooney amekuwa ni mchezaji wa nne wa United kukosa penati msimu huu ambapo meneja wake mzee Alex Ferguson mwenye umri wa miaka 70 amekuwa akijiuliza nani mwingine atakayepiga penati.

Katika hali ya utani mzee huyo akiongea na The Sun akasema
"Nadhani nitapiga mwenyewe wiki ijayo na nitafunga”.

Van Persie, Javier Hernandez na Luis Nani ni miongoni mwa wachezaji wengine waliokwisha kukosa penati msimu huu lakini Rooney anasema matokeo ya mchezo huo ndio yaliyokuwa muhimu zaidi.

“haya mambo huwa yanatokea na yamekwisha sasa".      
“ki ukweli nilihuzunika lakini ninasonga mbele na kwa kuwa tulishinda mchezo nadhani hilo lilikuwa muhimu zaidi.”

QPR haistahili kuwepo chini katika msimamo wa ligi anasema Cisse.

Mshambuliaji wa QPR Djibril Cisse amesema timu yake ina ubora na nzuri licha ya kushindwa kushinda katika jumla ya michezo ya 10 ya ligi msimu huu na jana kwenda sare ya bao 1-1 kule Loftus Road dhidi ya Reading.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa wa Ufaransa alifunga goli la kusawazisha kwa wenyeji hao wa mchezo huo wa jana katika kipindi cha pili ambapo waliutawala mchezo licha ya kushinda kuibuka na ushindi na ambapo wamejiweka katika  nafasi ya 19 katika msimamo wa ligi juu ya Southampton kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 amesisitiza kuwa kikosi chake kina ubora wa kuweza kupanda juu katika msimamo wa ligi kuu ya England na kuepuka kuwepo katika eneo la hatari lakini pia akisema wanapaswa kusahau majina na kuongea na kuanza kumalizia nafasi wanazotengeneza za ufungaji ili kujinasua na kuwa salama.

Amenukuliwa Sky Sports akisema,
"tulikuwa na fursa ya kushinda. Kama unapata nafasi ya wazi ya kufunga unapaswa kufunga. Hicho ndicho tunachokikosa kwasasa lakini tunaendelea kujaribu"

 "ubora tulionao katika timu hatustahili kuwepo chini katika msimamo, hatuheshimiwi na timu nyingine lakini hatustahili kuwepo pale.

"mpira unachezwa uwanjani na si majina au kuongea. Tunapaswa kufanya hivyo kila mchezo."

 Manchester City haija iva kutwaa tali la ligi ya mabingfwa ulaya anasema Mancini.

Meneja wa Manchester City Roberto Mancini amesema ni wazi itawawia vigumu sana safari hii kwa timu yake kufuzu kutoka katika hatua ya makundi ya michuano ya vilabu bingwa Ulaya mwaka huu.

Mabingwa hao wa ligi kuu ya England kwasasa wako mkiano katika kundi lao, kundi ambalo linaonekana kuwa gumu kwao baada ya kupoteza kwa Real Madrid na Ajax kisha kupata sare dhidi ya Borussia Dortmund.

Wakati nafasi ya kufuzu ikiwa finyu kwao meneja huyo mwenye umri wa miaka 47 amekiri kuwa bado haamini kama kikosi chake kama kweli kiko katika uwezo wa kimashindano katika michuano hiyo.
Akiongea na Guardian amenukuliwa akisema, 
"sidhani kama tuko tayari kushinda taji la vilabu bingwa safari hii".

"kama tunasema tuko tayari basi haitoki moyoni. Katika michuano hii matokeo ya kushangaza yanaweza kutokea mwezi Februari na Machi lakini ni kwamba pia tuko katika kundi gumu mwaka huu kama ilivyokuwa mwaka jana.

"sisi ni timu nzuri lakini hatuko tayari kwa michuano hii kama ilivyo kwa timu nyingine. Chelsea ilijaribu kwa miaka 10 kushinda taji. Bila shaka ilikuwa timu bora ulaya mwezi May baada ya miaka 10 pengine walistahili. Walistahili kushinda miaka mitatu au minne iliyopita."

Licha ya ugumu huo ulio mbele yao, bado Mancini na kundi lake wanategemea kusonga mbele kusaka alama tisa muhimu katika jumla ya michezo iliyosalia.

No comments:

Post a Comment