KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, January 2, 2013

MAKAMU WA RAIS MAALIM SEIF KUZINDUA MICHUANO YA MAPINDUZI USIKU WA LEO.

 Makamu wa kwanza wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad anatarajiwa kufungua rasmi michuano ya kombe la mapinduzi inayotarajiwa kuanza rasmi hii jioni ya leo ambapo michezo miwili itapigwa katika uwanja wa Aman huko Zanzibar.

Katika mchezo wa kwanza Bandari watakuwa wakikutana na Tusker ya Kenya na mchezo wa usiku ambao hasa ndio wa uzinduzi utakuwa ni kati ya Simba na Jamhuri ya Pemba.
Maalimu Seif amealikwa na waandaaji wa michuano hiyo ambayo bingwa wake mtetezi ni Azam FC ya jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea kusheherekea miaka 49  ya mapinduzi ya Zanzibar michuano ambayo pia hufanyika kila mwaka .
Akiongea na Rockersports msemaji wa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo Farouk Karim amesema,
Tayari timu za Tusker, Jamhuri  ya Pemba na Simba zimekwisha kuwasili Zanzibar tangu jana na taarifa zinasema Azam , Coast Union na Mtibwa zinatarajiwa kuwasili huko hii leo . Tiketi zilizo arifiwa mapema kuwa zinatengenezwa nje ya nchi zimeshawasili na zimetoka nje ya nchi.
Forouk ametaja viingilio kuwa ni kwa mchezo wa kwanza jukwaa la Urusi 1000,mzunguko 2000, VIP 5000. Usiku 2000, 3000, VIP 10000.


No comments:

Post a Comment