KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, January 1, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Balotelli kumbe ni msukule wa sheikh Mansour, haondoki Man City ng'o. THEO WALCOTT anasema subirini kidogo nitawaambia naelekea wapi baada ya mkataba kwisha. Harry Redknapp atakufa na Joe Cole.PSG wanasema hawaja mtaka Ashley Cole na baada ya kuletwa Hugo Lloris, Cudicini achapa lapa LA GALAXY ya Marekani.


Mancini: Balotelli ni muhimu kwa mmiliki wa klabu.

Roberto Mancini amesisitiza kuwa Mario Balotelli atasalia katika klabu yake ya Manchester City kufuatia mmiliki wa klabu Sheikh Mansour kumsajili mtaliano huyo kutokana na kile alichokiita kama uwekezaji mkubwa katika klabu hiyo.

Balotelli hajaonyesha kiwango bora tangu kuanza kwa msimu huu, ambapo amefunga magoli 3 tu katika mashindano yote, jambo ambalo lilianzisha minong’ono ya chini chini kuwa mshambuliaji huyo huenda akaondoka ligi kuu ya England ‘Premier League’ na kuelekea Italia ‘Serie A’ kwa kigogo cha soka nchini humo AC Milan mwezi huu wa January.

Hata hivyo meneja Mancini ameweka wazi kuwa’

"Sheikh Mansour anampenda Balotelli kwakuwa anaamini anakipaji na analitangaza jina la City duniani"

"tunapaswa kukubali kuwa Mario alisaini kama uwekezaji mkubwa,  na hii si klabu ambayo inatupa mtaji wake kupitia dirishani

"nadhani Mario atasalia lakini huko baadaye itategemea na yeye mwenyewe"



Redknapp amethibitisha kumtaka Joe Cole.
 Bosi wa Queens Park Rangers Harry Redknapp amethibitisha kuwa ataongea na meneja wa Liverpool  Brendan Rodgers kuhusiana na usajili wa Cole.

Redknapp anamjua vema Cole tangu wakati huo wakiwa pamoja katika klabu ya West Ham, na baadaye kufanya vema katika timu ya taifa ya England.

Cole alikuwa katika mpango wa Redknapp tangu wakati huo akifundisha Tottenham, lakini kiungo huyo akaamua kuelekea kwa meneja Roy Hodgson katika klabu klabu ya Liverpool ambako bado hajafanikiwa kuonyesha mafanikio.



Leonardo akanusha mazungumza na Ashley Cole.

Mkurugenzi wa michezo wa Paris Saint-Germain, Leonardo amepuuza taarifa kuwa yuko katika jaribio la kumshawishi Ashley Cole aondoke Chelsea katika dirisha hilo dogo lililoanza hii leo barani ulaya.

Cole atakuwa huru baada ya mkataba wake kumalizika  Stamford Bridge mwishoni mwa msimu na bosi wa sasa Rafael Benitez alinukuliwa akiweka wazi katika moja ya mikutano yake na wandishi wa habari kwamba mlinzi huyo wa England ataondoka darajani majira ya kiangazi.


Hata hivyo baadaye alirekebisha kauli yake na kusema kuwa Cole ataendelea kusalia Chelsea mara baada ya mkataba kumalizika jambo ambalo si Cole mwenyewe wala Frank Lampard ambaye naye yuko katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake aliyekubaliana na masharti mapya ya kusalia hapo.


Kwasasa PSG ambayo inafanya kufuru kifedha katika matumizi ya usajili inanolewa na Carlo Ancelotti, ambaye huko nyuma alikuwa pamoja na Cole wakati huo akiifundisha Chelsea.

Leonardo pia amekanusha taarifa kuwa Wesley Sneijder anampango wa kujiunga PSG ambapo amesema katika nafasi yake tayari PSG inawachezaji watano

Hata hivyo klabu hiyo ambayo kwasasa inamilikiwa na wamiliki wapya wa Qatar Investment Authority, imeanzisha mpango wa kumtaka Lucas Moura akitokea Sao Paulo ambaye tayari ameshakubali kujiunga nao na huenda wengi wakafuata.



Cudicini aamua kuelekea Galaxy.
 Mlinda mlango wa Tottenham goalkeeper Carlo Cudicini ameamua kujiunga na LA Galaxy inayoshiriki ligi ya soka ya nchini Marekani MLS kwa mkataba wa miaka miwili.

Cudicini, mwenye umri wa miaka 39, alishindwa kurejea katika ubora wake wa kunyaka mipira kule White Hart Lane baada ya kupata ajali ya pikipiki ambayo ilimtengua kiuno na maumivu makali yaliyotona na kuumia mfupa wa nyonga.

Kufuatia kusajiliwa kwa Hugo Lloris na kupelekea yeye kuwa mlinda mlango namba tatu nyuma ya mlinda mlando mfaransa Brad Friedel ambaye hivi karibuni amesaini mkataba mpya, sasa Cudicini ameamua kutafuta mwelekeo mpya nchini Marekani.

Mtaliano huyo ameamua kuondoka kusaka namba nchini Marekani na inaarifiwa kuwa anakuwa ni miongoni mwa wachezaji wanaolipwa mshahara mnono.

Cudicini alijiunga White Hart Lane mwezi January 2009 kwa uhamisho huru baada ya kuidakia Chelsea miaka tisa na sasa anajiunga na mchezaji mwenzake wa zamani wa  Tottenham Robbie Keane katika klabu ya Galaxy.


Walcott: hatma yangu itafahamika hivi punde.
 Theo Walcott ameelezea juu ya hitajio lake la kutaka kusalia katika klabu yake ya Arsenal licha ya mshambuliaji huyo sasa kuwa anaweza kufungua mazungumzo na klabu nyingine.

Makataba wa Walcott wa sasa utafikia kikomo mwishini mwa msimu huu ambapo kwasasa majadiliano juu ya mkataba mpya yakitazamiwa kuanza baadaye mwezi huu.

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ana matumaini kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England atafuata nyayo za wachezaji wenzake vijana wa England Jack Wilshere, Alex Oxlade-Chamberlain, Aaron Ramsey, Kieran Gibbs na Carl Jenkinson ambao walisaini mikataba mipya muda kabla ya sikukuu ya Christmas.

Hata hivyo Wenger amesema mwezi uliopita alitarajia mambo hayo yangekuwa yamemalizwa kabla ya mwaka mpya.

Licha ya songombingo hiyo, bado Walcott anasisitiza kuwa anataka kusalia Emirates Stadium.

Amenukuliwa na The Sun akisema

“nina imani kila kitu kitakwenda vizuri hivi karibuni"

“siku zote nimekuwa nikisema kuwa nataka kusalia na kufurahia kucheza katika timu hii. Hebu tuone nini kitafuata”

Kwa mujibu wa sheria za uhamisho ni kwamba kwasasa  Walcott anaweza kusaini mkataba wa awali na klabu nyingine yoyote ya nje ambayo atapenda mpaka mkataba wake utakapo kwisha rasmi mwezi June ambako ambako atasaini kama mchezaji huru.

No comments:

Post a Comment