KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, September 6, 2013

Licha ya kumsajili Bale kwa dau kubwa la dunia, Real Madrid yatangaza faida.

 
 
Siku chache tu baada ya kutumia kitita kikubwa kumsajili Gareth Bale kutoka klabu ya Tottenham hotspurs ya England Real Madrid imetangaza kupanda kwa faida katika mapato yake na punguzo la asilimia 27.4 ya deni lake katika kipindi cha msimu wa mwaka 2012/13.
 Magwiji hao wa soka ya Uhispania wameshuhudia mapato yao yakipanda mpaka kufikia Euro milioni 520.9.

Mapato hayo hayahusishi udhamini mkubwa wa Fly Emirates wa shati za klabu unaokadiriwa kuwa euro milioni 29 kwa kila mwaka kuanzia msimu huu.

Pamoja na usajili wa Bale, Real ilitumia euro milioni 70 kwa kuwapata Isco na Asier Illarramendi.

Vilevile klabu hio ilirejesha takriban euro milioni 100 katika kuwauza wachezaji wake Mesut Ozil aliyejiunga na Arsenal kunako siku ya mwisho wa usajili na Gonzalo Higuain, Raul Albiol na Jose Maria Callejon waliojiunga na Napoli mwezi julai.

Uwamuzi wa Kaka kuondoka Real Madrid na kurudi AC Milan pia kulipunguza kiwango cha mishahara ya klabu hiyo kwa mshahara wake wa euro milioni 10 kwa mwaka wake wa mwisho lau kama angehitimisha mkataba wake.

No comments:

Post a Comment