Mlinzi wa Azam fc ya jijini Dar es Salaam Jockins Atudo kwa mara nyingine amethibitisha ubora wake wa kuwa kikosini Harambee Stars ya Kenya baada ya kufunga bao muhimu kupitia mkwaju wa penati na kuipeleka timu yake katika nusu fainali ya michuano ya Chalenji.
Atudo, mfungaji wa bao pekee dhidi ya Rwanda amefikisha mabao matatu katika viwanja vitatu tofauti ambavyo Kenya walikuwa wakitumia kuanzia hatua ya makundi.
Amefunga mabao hayo katika uwanja wa Nyayo, Nakuru na leo Mombasa Stadia.
Sasa Kenya watakutana dhidi ya Kilimanjaro Stars ambao wamewaondosha mashindanoni mabingwa mara 13 Uganda kwa mikwaju ya penati.
No comments:
Post a Comment