KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, January 1, 2014

Dk Shein: Tujenge na kuuendeleza utamaduni wa kufanya mazoezi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Wanamichezo wa Vikundi vya Mazoezi ya Viungo katika Bonanza la 5,Vikundi vya mazoezi ya Viungo,lililofanyika katika Uwanja wa Amaan,Wilaya ya Mjini Unguja,katika shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]


STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

    Zanzibar                                                                     01 Januari, 2014


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi kujenga na kuendeleza utamaduni wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao pamoja na kujikinga na maradhi yanayoweza kuepukika.
Dk. Shein ametoa kauli hiyo leo wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa klabu za mazoezi na vyama vya michezo katika Bonanza Maalum la Mazoezi ya Viungo lililofanyika katika uwanja wa Amaan mjini Unguja.
Kabla ya kuzungumza na wanamichezo hao Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akiwa amefuatana na Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi pamoja na viongozi wengine walioshiriki matembezi ikiwa ni sehemu ya Bonanza hilo yaliyoanzia Michenzani mjini Unguja hadi Uwanjani hapo.
Dk. Shein aliwaeleza washiriki kuwa ni jambo lililo dhahiri kuwa kufanya mazoezi ni jambo la msingi sana katika kuimarisha afya ya mwili na kuchangamsha akili hivyo Serikali ina kila sababu ya kuziunga mkono jitihada walizozianzisha za kuunda vikundi vya mazoezi.
Alifafanua kuwa hivi sasa kumekuwepo na maradhi mengi ambayo hapa kwetu yanaelezwa kusababishwa na mabadiliko ya mtindo wa maisha na kuyataja maradhi hayo kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, kisukari na kuongezeka unene ambayo yanaweza kupunguza kwa kufanya mazoezi.

Pichani chini Dr Shein akiongoza matembezi ya Bonanza la vikundi vya mazoezi ya viungo

Kikundi cha Brassband cha Mafunzo kikiwa mbele ya Matembezi ya Bonanza la 5 la Vikundi vya Mazoezi ya Viungo,yanayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,na viongozi mbali mbali wakishiriki,matembezi hayo yameanzia Uwanja wa Kisonge,hadi uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,(katikati) na viongozi mbali mbali walioshiriki,Matembezi ya Bonanza la 5 la Vikundi vya Mazoezi ya Viungo, yaliyoanzia Uwanja wa Kisonge,hadi uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja,
Wanavikundi vya mazoezi ya Viungo wa Zone A,wakiwa katika Matembezi ya Bonanza la 5,yanayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,na viongozi mbali mbali wakishiriki,matembezi hayo yaliyoanzia Uwanja wa Kisonge,na kumalizia Uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja
Kikundi cha Mazizini Beach Exercise Group,hawakuwa nyuma katika Matembezi ya Bonanza la 5,yanayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,na viongozi mbali mbali wakishiriki,matembezi hayo yaliyoanzia Uwanja wa Kisonge,na kumalizia Uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja
Kikundi cha Training & Fitness Obama Club,wakiwa katika Matembezi ya Bonanza la 5,yanayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,na viongozi mbali mbali wakishiriki,matembezi hayo yaliyoanzia Uwanja wa Kisonge,na kumalizia Uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja
Kikundi cha Mchezo wa Judo,wakiwa katika Matembezi ya Bonanza la 5,yanayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein,na viongozi mbali mbali wakishiriki,matembezi hayo yaliyoanzia Uwanja wa Kisonge,na kumalizia Uwanja wa Amaan Wilaya ya Mjini Unguja

No comments:

Post a Comment