KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 22, 2012

Leopards yatinga nusu fainali ya Confederation Cup



AC Leopards imekuwa ni klabu ya kwanza kutoka Congo Brazzaville kutinga nusu fainali ya michuano ya Confederation barani Afrika baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Djoliba ya Mali mchezo ulichezwa Jumapili.
Leopards, yenye maskani yake katika mji wa magharibi wa Dolisie, walihitaji matokeo ya kama ya Wydad Casablanca ya Morocco katika dimba la Stade Malien kule Mali kujihakikishia usalama wa nafasi ya pili nyuma ya washindi wa kundi B Djoliba.
Casablanca ilikwenda sare ya bao 3-3 Stade baada ya kuwa na kazi ya kusawazisha mara tatu wakitokea nyuma kimatokeo.
Historia inaonyesha kuwa hakuna klabu kutoka Afrika ya kati iliyokaribia kushinda taji hilo tangu CARA ya Brazzaville kufanikiwa kufanya hivyo mara ya mwisho 38 iliyopita.

Gedo aiongoza  Al Ahly kutinga fainali ya mabingwa Afrika
Bao la kipindi cha kwanza kupitia kwa Gedo lilitosha kuwapa ushindi Al Ahly na kutinga fainali ya vilabu bingwa Afrika baada ya kigogo hicho cha soka barani Afriaca kuichapa Sunshine Stars ya Nigeria.
Ushindi huo wa Ahly wa bao 1-0 umewapa ushindi wa jumla wa mabao 4-3 na sasa wanatarajia kukutana dhidi wapinzani wao wakubwa katika ukanda wa kaskazini Esperance mwezi ujao.
Bao lilitoka na mpira wa shuti uliompoteza mlinda mlango Moses Ocheje kunako dakika ya 28 na hivyo kukamilisha safari ya fainali ya Ahly baada ya mchezo wa kwanza kumalizika kwa sare ya bao 3-3 nchini Nigeria wiki mbili zilizopita.
Mchezo huo ulichezwa bila ya watazamaji kwa sababu za kiusalama baada ya vurugu za mwezi wa pili ambapo pia  Ahly ilitawala mchezo katika sehemu kubwa ya mchezo huo.

Gerrard: Namkubali Sterling anaweza kufiki mbali 
Nahodha wa Liverpool na timu ya taifa ya England Steven Gerrard anadhani Raheem Sterling anaweza kufika mbali kimafanikio baada ya kuanza vizuri katika uchezaji wake timu za wakubwa.
Kinda huyo mwenye umri wa miaka 17 alifunga goli lake la kwanza kwa Liverpool mwishoni mwa juma katika mchezo dhidi ya Reading, na kuwa mchezaji wa pili chipukizi katika historia ya Liverpool kufunga goli.
Amenukuliwa Gerrard akisema
"nadhani ni mtu anaye mshangaza kila mtu, si kwasababu anafanya vizuri katika kiwango hiki lakini pia hakuna anayedhani kuwa uwezo wake utakwisha mapema, nafikiri kila mtu anajua kuwa ndio kwanza anaanza kuchezea timu ya wakubwa wakati mwingine inabidi kuwa mwangalifu”
Gerrard anaamini kuwa Brendan Rodgers ana imani na Sterling na kwamba ana kuwa ni sehemu muhimu katika maendeleo yake lakini pia Gerrad akaonya kuwa kocha huyo wa zamani wa QPR bado anasafari ndefu.

No comments:

Post a Comment