Atletico Madrid imeweka wazi kuwa kocha wake mkuu Diego Simeone amesaini makataba mpya na klabu hiyo utakao muweka ndani ya klabu hiyo mpaka 2017.
Mkataba wa sasa wa muajentina huyo unatarajiwa kumalizika mwishoni kwa msimu huu na hapo kabla ilielezwa kuwa mipango ya baadaye ingetegemea shughuli za uhamisho za majira ya kiangazi.
Simione ameingoza Atletico mpaka kushika nafasi ya pili katika La Liga, na sasa kuelekea katika fainali ya Copa del Rey, amesaini mkataba wa muda mrefu.
No comments:
Post a Comment