KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, August 2, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: SOLDADO ANASEMA SI RAHISI KUCHEZA NA GARETH BALE, REDKNAPP ANASEMA HATA KAMA UNAMTAKA REMY KWA MKOPO LIPA KWANZA PAUNI MILIONI 2, RONALDO KUMBE NI KIRAKA NDANI YA MADRID, BALE BADO KIDUCHU KUTUA MADRID. SUAREZ KUTIMKA TU.


MSHAMBULIAJI  wa Liverpool anayegonga vichwa vya habari kila kukicha, Luis Suarez, imearifiwa kuwa hataendelea kusalia kunako klabu hiyo na badala yake ataamua  kuhamia Arsenal, hii ikiwa kauli ya mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Ian Wright.

Liverpool inashikilia msimamo wake wa kutotaka kumuuza Suarez kiasi cha kuwafurusha mara mbili Arsenal na ofa ya kutaka kumsajili mchezaji huo, anayetaka kujiunga na klabu inayoshiriki ligi ya mabingwa ulaya msimu huu.
 
Suarez raia wa Uruguay nchi ambayo imepitisha muswaada wa kuhimiza wananchi kulima kwa wingi zao la bangi, ameshaweka wazi kuwa anataka kuondoka Liverpool licha kuingia kandarasi ya muda mrefu na klabu hiyo tangu mwaka, 2012.

Ian Wright, anaamini kuwa ofa mpya ya pauni milioni 41 iliyotolewa na Arsenal itaweza kumfanya suarez kukubali kujiunga na wabeba mitutu hao wa London, lakini Liverpool inataka kumruhusu mchezaji huyo kuondoka endapo itajitokeza klabu yenye uwezo wa kulipa pauni milioni 50.

………………………………
Katika hatua nyingine Liverpool, imetoa ofa ya pauni milioni £21kuelekea katika klabu ya Atletico Madrid ya Hispania, kwa lengo la kumsajili mshambuliaji wao Diego Costa.


Ofa hiyo inaaminika kuwa huenda ikakubaliwa na uongozi wa Atletico Madrid na kumruhusu Costa, 24 kuondoka,na kocha wa  Liverpool, Brendan Rodgers,anamatumaini kuwa watakamilisha dili hilo bila matatizo.

Costa, ambaye ni raia wa nchini Brazil, alijiunga na Atletico Madrid mwaka 2010 akitokea klabu ya Valladolid, na amefanikiwa kufunga mabao 10 kwenye michuano ya ligi kuu ya Hispania msimu uliopita.

...........MWISHO.......

MOHAMED KALLON AENGELUWA UCHAGUZI WA URAIS WA SOKA NCHINI SIERA LEONE. 
 Shirikisho la mpira wa miguu duniani Fifa, limekubaliana na uamuzi wa kuenguliwa kwa Mohamed Kallon na watu wengine wawili, Rodney Michael na Foday Turay, katika kinyang’anyiro cha urais wa shirikisho la kandanda la Sierra Leone.

Hii inamaanisha kuwa, mwana mama Isha Johansen, aliyetimiza vigezo vyote vinavyohitajika katika kuwania nafasi hiyo, atakuwa mgombea pekee wa urais wa shirikisho hilo la mpira nchini Siera Leone, na atakuwa Rais wa kwanza mwanamke kuongoza shirikisho hilo.

Uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo nchini sierra leone, SLFA,unataraji kufanyika mapema kesho jumamosi.

Mohamed Kallon,ambaye ni mshambuliaji  wa zamani wa vilabu vya Inter Milan na AS Monaco, ameenguliwa katika kinyang’anyiro hicho baada ya shirikisho kujiridhisha kuwa hakuwepo nchini humo kwa zaidi ya miaka 5, ikiwa ni sifa moja wapo inayohitajika kuwa mgombea wa nafasi hiyo.

Hata hivyo Kallon, mwenyewe amekanusha madai hayo akisema kuwa hayana ukweli wowote na maamuzi hayo ni uonevu mtupu kwake.

...................MWISHO..............

 The Cranes kujipima kwa Mapharao wa Misri.
Timu ya taifa ya Misri itakutana uso kwa uso dhidi ya timu ya taifa ya Uganda 'The cranes', katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki utakaopigwa tarehe 14 ya mwezi huu, mchezo ambao kwa timu zote mbili utatumika kama maandalizi ya michuano ya kufuzu kombe la dunia.

Mchezo huo utafanyika katika mji wa Pwani wa El Gouna,  kilometa 430 toka jijini Cairo, kutokana na kuepuka vurugu za vuguvugu la kisiasa na kiusalama.

Makamu wa rais wa shirikishao la soka nchini Uganda, Mujib Kasule, amesema mchezo huo ni muhimu ili kujiweka fiti kwa timu zote mbili na kutoa nafasi kwa makocha kuona mapungufu ya vikosi vyao.

Naye kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uganda, Milutin 'Micho, amethibitisha kuwa mchezo huo utaisadia kuiwashia taa ya kijani kuelekea katika michuano ya kombe la dunia.

The Cranes ipo katika nafasi ya pili kwenye kundi lao ikiwa na pointi 8, ambapo italazimika kuwafunga vinara wa kundi, Senegal tarehe 7 mwezi September, mchezo ambao utafanyika mjini Marrakech, nchini Morocco.

Wakati wamisri wao, tayari wakiwa wamefuzu  katika raundi inayofuata ya michuano ya kufuzu kombe la dunia mwakani, baada ya kujinyakulia pointi 15 kwenye kundi lao la G, wakati nafasi ya pili ikishikiliwa na Guinea yenye pointi  10.

............MWISHO.........

  SOLDADO ANASEMA SI RAHISI KUCHEZA NA GARETH BALE
 Mchezaji mpya aliyesajiliwa na klabu ya Tottenham
Hotspur, Roberto Soldado, amekiri kuwa hatarajii kucheza pamoja na kiungo Gareth Bale, kwa kuwa mchezaji huyo safari yake imeiva.

Tottenham Hotspur imemsajili Soldao kwa ada ya kuvunja rekodi ya usajili ya klabu hiyo ,pauni milioni £26m,ili kuimarisha safu yake ya uishambuliaji kabla ya kuanza michuano ya ligi.

Soldado,amesema anapenda kuona anakwenda kwenye timu Spurs ambayo Bale anacheza,lakini asingependa kuona wanapangwa pamoja.

Soldado aliyetokea klabu ya Valencia,alijiunga na klabu hiyo akitokea Getafe miaka mitatu iliyopita amefanikiwa kufunga mabao  80 katika mechi 146,ikiwemo magoli  24 aliyoyafunga msimu uliopita wa ligi ya La Liga.

Anakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Spurs katika usajili huu wa majira ya joto,na atakamilisha zoezi hilo la usajili wake leo ijumaa baada ya kufanyiwa vipimo vya afya yake.

Wachezaji wengine waliosajiliwa na Spurs majira haya ya joto ni pamoja na kiungo Paulinho toka klabu ya Corinthians ya brazil kwa ada ya pauni milioni £17m,pamoja na Nacer Chadli toka klabu ya FC Twenty kwa ada ya karibu pauni milioni £7m.

Kocha mkuu wa klabu ya Valenci,Miroslav Duckic,amesema uongozi wa klabu yake baada ya kushindwa kuipata saini ya mshambuliaji wa Aresenal,Olivier Giroud na mshambuliaji wa klabu ya Real Zaragoza-Helder Postiga,umeamua kuelekeza juhudi zao kuifukuzia saini ya Fernando torres wa Chelsea.

.........Mwisho..........

 REDKNAPP ANASEMA HATA KAMA UNAMTAKA REMY KWA MKOPO LIPA KWANZA PAUNI MILIONI 2
Kocha wa klabu ya QPR, Harry Redknapp, amesema klabu yeyote itakayojitokeza kutaka kumchukua mshambuliaji wao  Loic Remy kwa mkopo, italazimika kuweka mezani pauni milioni  £2m.

Tayari Newcastle  united,ipo katika mazungumzo na QPR,kuhusu mchezaji huyo aliyejiunga nao tangu mwezi januari kwa ada ya pauni milioni £8m.

 ‘huyu ni mchezaji ambaye tumekubaliana kuwa tutamtoa kwa mkopo,lakini klabu ambayo inahitaji huduma yake ni lazima itoe pauni milioni mbili,lakini kama ipo klabu inayotaka kumnunua moja kwa moja basi italazimika kutoa pauni milioni £8million.

.......MWISHO........

 RONALDO KUMBE NI KIRAKA NDANI YA MADRID.
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema kuwa mshambuliaji wake nyota  Cristiano Ronaldo, anaweza kucheza katika nafasi yeyote atakayoitaka,hii ni katika kile kinachoonekana klabu hiyo kutaka kumbakiza asiondoke.

Taarifa za mwisho jioni hii zinasema, tayari mabingwa wa England Manchester united, wameanza mazungumzo na uongozi wa Madrid ili kumrejesha Ronaldo Old Trafford.

Lakini kocha Ancelotti, aliyechukua mikoba ya kukiongoza kikosi hicho hivi karibuni, anahaha kutaka kumbakisha ronaldo lakini kama ataamua kuondoka, basi atalazimika kuingia katika vita ya kumfukuzia kiungo wa Tottenham, Gareth Bale ili amjumuishe kwenye kikosi chake .

..........MWISHO.......

 BALE BADO KIDUCHU KUTUA MADRID
Klabu ya Tottenham inakaribia kabisa kukubali kumuuza nyota wao anayekipiga pia na timu ya taifa ya  Wales, Gareth Bale,kwa dau la pauni milioni 105 ambalo  Real Madrid,wamekubali kutoa.

Kocha wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti, amethibitisha kuwa klabu yake ipo katika mazungumzo mazito na ya mwisho kabisa na uongozi wa Tottenham,kuhusu dili hilo.

Bale, 24,yupo chini ya uangalizi wa madaktari ambao wanampatia matibabu madogo baada ya kuumia,na huenda akakosa mechi mbili za mwisho za kujiandaa na msimu wa ligi kuu.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment