Matumaini ya Arsenal ya kumsajili Sami Khedira kipindi huki cha usajili yamegonga mwamba kufuatia kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti kuthibtisha kuwa kiungo huyo ataendelea kusalia nchini Hispania.
Washika mitutu walikuwa wakiaminika kuwa katika maandalizi ya uhamisho wa Mjerumani huyo kwa pauni milioni 12 wiki hii kufuatia Ancelotti hivi karibuni kudai kuwa kiungo huyo alikuwa huru kusaka muelekeo mpya.
Lakini kocha huyo Mtaliano mwenye umri wa miaka 55 sasa anakanusha kutaka kumuuza Khedira kipindi hiki.
Ananukuliwa akisema
‘Khedira anafuraha hapa, na atasalia hapa, mambo yamewekwa sawa na sasa anaendelea hapaReal Madrid,’ Amesema Ancelotti.
No comments:
Post a Comment